sw_tn/isa/22/20.md

1.4 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza ujumbe wa Mungu kwa Shebna.

Itakuja kuwa katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi kwa ujumla. "'Itatokea katika kipindi hicho"

Eliakimu ... Hilkia

Haya ni majina ya wanamume.

Nitamvisha kwa gwanda lako na kumwekea juu yake mshipi wako

Yahwe kusababisha Eliakimu kuchukua nafasi ya Shebna katika kasri ya mfalme inazungumziwa kana kwamba Yahwe atamvisha Eliakimu katika nguo za Shebna ambazo zinawakilisha mamlaka yake katika kasri ya mfalme.

gwanda lako ... mshipi wako

Hapa gwanda na mshipi inawakilisha mamlaka katika kasri ya mfalme.

mshipi

Hii ni kipande cha nguo ambacho watu huvaa kuzunguka kiuno au kupita kifuani.

katika mkono wake

Hapa "mkono" unawakilisha nguvu na utawala. "kwake"

Atakuwa baba

Eliakimu kutunza na kulinda watu wa Yuda inazungumziwa kana kwamba angekuwa baba yao. "Atakuwa kama baba"

katika nyumba ya Yuda

Hapa "nyumba" inawakilisha watu. "kwa watu wa Yuda"

Nitaweka ufunguo wa nyumba ya Daudi juu ya bega lake ... hakuna atakayefungua

Hapa "ufunguo" inawakilisha mamlaka. Hii inazungumzia Eliakimu kuwa na mamlaka ambayo hakuna mtu awezaye kumzuia kana kwamba alikuwa na ufunguo wa kasri na hakuna mtu mwingine awezaye kufunga au kufungua mlango. "Nitamweka kuwa msimamizi wa wale ambao hufanya kazi katika kasri ya mfalme, na anapofanya maamuzi hakuna atakayeweza kumpinga"