sw_tn/isa/16/06.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea katika siku za usini kana kwamba yanatokea katika wakati wa sasa.

Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu, majivuni yake, kujidai kwake, na hasira yake

Maneno haya "cha Moabu" na "yake" yana maana ya watu wa Moabu. "Tumesikia ya kwamba watu wa Moabu wana kiburi na majivuni, wanajidai na wana hasira"

Tumesikia

Maana zaweza kuwa 1) Isaya anazungumza na "Tumesikia" ina maana ya kwake na watu wa Yuda, au 2) Mungu anazungumza na "Tumesikia" ina maana ya Mungu.

Lakini kuringa kwake ni maneno matupu

"Lakini kile wanachosema kuhusu wao haina maana yoyote" au "Lakini kile wanachojidai nacho sio cha kweli"

Kwa hiyo Moabu anaomboleza kwa ajili ya Moabu - wote wanaomboleza

"Moabu" inawakilisha watu wa Moabu. "Kwa hiyo watu wa Moabu watalia kwa sauti juu ya kile kilichotokea kwa miji yao"

kwa maana keki ya zabibu kavu ya Kir-Haresethi

"kwa sababu hakuna keki za zabibu kavu katika Kir-Haresethi"

keki ya zabibu kavu

Neno la Kiebrania linalotumiwa hapa lina maana aidha ya "keki ya zabibu kavu" au "wanamume".

Kir-Haresethi

"Kir-Haresethi" ni jina la mji.