sw_tn/isa/15/05.md

875 B

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea katika muda ujao kana kwamba yanatokea katika wakati wa sasa.

Moyo wangu unalia kwa ajili ya Moabu

Moyo unawakilisha hisia. Mungu anazungumzia huzuni yake kubwa kana kwamba moyo wake ulilia kwa sauti. "Nina huzuni sana juu kile kinachoendelea Moabu"

wakimbizi wake hutoroka

"wakimbizi kutoka Moabu watatoroka". Mkimbizi ni mtu ambaye hutoroka ili kwamba adui zake wasiweze kumkamata.

Soari ... Eglathi Shelishiya ... Luhithi ... Horonaimu ... Nimrimu

Haya ni majina ya miji mikubwa na miji midogo.

juu ya uharibifu

Hii inaweza kuelezwa ili kwamba nomino dhahania "uharibifu" inaelezwa kama kitenzi "kuangamizwa". "kwa sababu mji wao umeangamizwa"

wingi

"Kila kitu"

kijito cha mipopla

Hii inaweza kumaanisha mto katika mpaka wa kusini wa Moabu.