1.1 KiB
Taarifa ya Jumla
Mara kwa mara katika unabii, matukio yajayo yanaelezwa kama yanatokea sasa au katika kipindi cha nyuma. Hii inasisitiza ya kwamba tukio hakika litatokea.
Tamko
"Hiki ni kile ambacho Yahwe anatamka" au "Huu ni ujumbe utokao kwa Yahwe"
Ari ... Kiri ... Diboni ... Nebo ... Medeba
Haya ni majina na miji ya Moabu.
Ari ya Moabu imewekwa kama takataka na kuangamizwa
Maneno "imewekwa kama takataka" na "kuangamizwa" ina maana moja na inasisitiza ya kwamba mji uliharibiwa kabisa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Majeshi ya adui yataangamiza kabisa Ari ya Moabu"
kwenda juu kileleni kulia
Hapa "juu kileleni" ina maana ya katika hekalu au dhabahu ambalo limejengwa juu ya nchi kama kilima au upande wa mlima. "kwenda juu hekaluni juu ya juu ya kilima kulia"
Moabu huomboleza juu ya Nebo na juu ya Madeba
Majina ya sehemu hizi ina maana ya watu wanaoishi kule. "watu wa Moabu watalia kwa sababu ya kile kilichotokea kwa miji ya Nebo na Medeba"
Vichwa vyao vyote vimenyolewa wazi na ndevu zao zote zimekatwa
Wanafanya hivi kuonyesha huzuni yao kuu. "Wote watanyoa vichwa vyao na kukata ndevu zao na kuhuzunika"