sw_tn/isa/15/01.md

1.1 KiB

Taarifa ya Jumla

Mara kwa mara katika unabii, matukio yajayo yanaelezwa kama yanatokea sasa au katika kipindi cha nyuma. Hii inasisitiza ya kwamba tukio hakika litatokea.

Tamko

"Hiki ni kile ambacho Yahwe anatamka" au "Huu ni ujumbe utokao kwa Yahwe"

Ari ... Kiri ... Diboni ... Nebo ... Medeba

Haya ni majina na miji ya Moabu.

Ari ya Moabu imewekwa kama takataka na kuangamizwa

Maneno "imewekwa kama takataka" na "kuangamizwa" ina maana moja na inasisitiza ya kwamba mji uliharibiwa kabisa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Majeshi ya adui yataangamiza kabisa Ari ya Moabu"

kwenda juu kileleni kulia

Hapa "juu kileleni" ina maana ya katika hekalu au dhabahu ambalo limejengwa juu ya nchi kama kilima au upande wa mlima. "kwenda juu hekaluni juu ya juu ya kilima kulia"

Moabu huomboleza juu ya Nebo na juu ya Madeba

Majina ya sehemu hizi ina maana ya watu wanaoishi kule. "watu wa Moabu watalia kwa sababu ya kile kilichotokea kwa miji ya Nebo na Medeba"

Vichwa vyao vyote vimenyolewa wazi na ndevu zao zote zimekatwa

Wanafanya hivi kuonyesha huzuni yao kuu. "Wote watanyoa vichwa vyao na kukata ndevu zao na kuhuzunika"