sw_tn/isa/14/21.md

2.2 KiB

Andaa machinjio yako kwa ajili ya watoto wake

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "machinjio" ilelezwa kwa kitenzi "ua"."Jiandae kuwaua watoto wa mfalme wa Babeli"

kwa maana udhalimu wa mababu zao

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "udhalimu" inaelezwa kama kitenzi "tenda dhambi sana". "kwa sababu babu zao walitenda dhambi sana"

ili wasiweze kuinuka juu

Hapa "kuinuka juu" inawakilisha aidha kuwa na nguvu au kushambulia. "ili wasiweze kuwa na nguvu" au "ili wasishambulie"

kumiliki dunia

Hii inawakilisha kutawala juu ya watu wa dunia, katika suala hili kwa kuwashinda wao. "tawala juu ya watu wa dunia" au "washinde watu wa dunia"

na kuijaza dunia nzima kwa miji

Hii inawakilisha kusababisha dunia kuwa na mijij mingi. "na kujenga miji duniani kote"

Nitainuka juu dhidi yao

Hii ina maana ya kwamba Mungu atafanya jambo dhidi yao. neno "yao" lina maana ya watu wa Babeli. "Nitawashambulia" au "Nitatuma watu kuwashambulia"

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "tamko" lielezwa kama kitenzi "tamka" au "sema kwa dhati". "hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyotamka" au "hivi ndivyo kile Yahwe wa majeshi alivyosema kwa dhati"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi wa Israeli.

Nitakata jina la Babeli, uzao, na watoto

"Kukata" inawakilisha kuangamiza. Hapa "Babeli" ina maana ya watu wa Babeli. Pia, "jina" ina maana ya aidha umaarufu wa Babeli au Babeli yenyewe kama ufalme. "Nitaangamiza Babeli, pamoja na watoto wa watu na wajukuu"

Pia nitaifanya

Neno "nitaifanya" ina maana ya mji wa Babeli. Miji mara kwa mara ilizungumziwa kana kwamba ilikuwa wanawake. "Pia nitaifanya"

milki ya bundi

Hii inawakilisha wanyama pori wanaoishi katika mji kwa sababu hakuna watu pale. "sehemu ambayo bundi huishi" au "sehemu ambayo wanyma pori huishi"

na kuwa dimbwi za maji

Kusababisha kuwepo vinamasi au madimbwi ya maji yaliyotulia ambapo mji ulikuwepo inazungumziwa kama kufanya mji kuwa vitu hivyo. "na katika sehemu ambapo kuna madimbwi yaliyotulia"

nitaifagia kwa ufagio wa uharibifu

Hii inawakilisha kuangamiza Babeli kabisa na kuifanya isiwepo tena kana kwamba ilikuwa uchafu usiokuwa na thamani ambao watu hufagia. "Nitaangamiza kabisa, kama kufagia kwa ufagio"