sw_tn/isa/10/10.md

1.1 KiB

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kunukuu kile mfalme wa Ashuru anachosema.

Kama mkono ulivyoshinda

"Mkono" ni kumbukumbu kwa nguvu ya jeshi. "Kama jeshi langu lenye nguvu lilivyoshinda" au "Kama nilivyoshinda"

wangu

Hii ina maana ya mfalme wa Ashuru.

ambao sanamu zao za kuchonga zilikuwa kubwa kuliko

Katika kipindi hiki watu waliamini ya kwamba ukubwa wa sanamu ulionyesha jinsi ufalme ulivyokuwa na nguvu ambayo iliijenga. Mfalme wa Ashuru kusema kuwa kwa sababu sanamu katika Yerusalemu sio kubwa kama sanamu za falme alizozishinda, Yerusalemu ingekuwa na uwezo mdogo zaidi kumshinda kuliko zingine.

kama nilivyofanya kwa Samaria na sanamu zake sizizo na thamani

Neno "Samaria" lina maana ya watu ambao waliishi pale, na "zake" ina maana ya mji wa Samaria. Miji na mataifa mara kwa mara ilizungumziwa kana kwamba ilikuwa wanawake. "'kama nilivyofanya kwa watu wa Samaria na sanamu zao sizizo na thamani"

sitafanya hivyo hivyo pia kwa Yerusalemu na kwa sanamu wake?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali kusisitiza uhakika ya kwamba atashinda watu wa Israeli. "Hakika nitafanya kile kile kwa Yerusalemu na sanamu wake!"