sw_tn/isa/10/05.md

1.7 KiB

Ole

neno hili linaweka alama mwanzo wa tangazo la Mungu kuhusu adhabu kali dhidi ya Ashuru.

Ashuru

Hii ina maana ya mflame wa Ashuru.

rungu ya hasira, fimbo ambayo ninatawala ghadhabu yangu

Misemo hii miwili ina maana moja. Yahwe analinganisha mfalme wa Ashuru kwa silaha ambayo mtu hubeba mkononi na kupiga watu wengine. Inasisitiza ya kwamba mfalme wa Ashuru na jeshi lake ni chombo ambacho Yahwe hutumia kuadhibu Israeli. "nani atakuwa kama silaha mikononi mwangu ambayo nitaitumia kuponyesha hasira yangu"

ninamtuma ... ninamuamuru

Neno "ninamtuma" hapa pia ina maana ya mflame wa Ashuru. Lakini haimaanishi Mungu anamtuma mfalme pekee; anamtuma pamoja na jeshi la Ashuru. "Ninatuma jeshi la Ashuru ... ninawaamuru"

dhidi ya taifa lenye kiburi na dhidi ya watu ambao wanabeba ghadhabu yangu ya kumwagikia

"kushambulia taifa lililojaa watu wenye kiburi ambao wamenifanya niwe na hasira sana"

ambao wanabeba ghadhabu yangu ya kumwagikia

Yahwe anazungumzia ghadhabu yake kana kwamba ilikuwa kimiminiko kuzidi chombo ambacho kilibeba; "watu" wanajaribu kubeba chombo chake, lakini ni kizito, na Yahwe anamwaga kimiminiko ndani hata baada ya kuanza kumwagikia nje. "ambao ninaendela kuwa na hasira nao hata baada ya kuwaadhibu"

kuchukua mateka

"kuchukua kila kitu walichonacho"

kuchukua mawindo

kuwachukua watu kama mawindo.

kuwakanyaga kama tope

Maana zaweza kuwa 1) Yahwe analinganisha jeshi la Ashuru kushambulia Israeli na watu kukanyaga katika tope ambao hawajali nini kinatokea kwa matope. "wakanyage mpaka wawe kama matope" au 2) watu wanakanyaga juu ya watu wengine kwa hiyo wanalala kwenye matope na kushindwa kuinuka. Hii ni sitiari ya kuwashinda kabisa. "kuwashinda kabisa"