sw_tn/isa/10/01.md

823 B

kwa wale ambao hufanya sheria zisizo za haki na kuandika maagizo yasiyo ya haki

Misemo hii miwili ina maana moja. "kwa wale ambao hutengeneza sheria na maagizo ambayo sio haki kwa wote"

Watawanyima wahitaji haki, kunyanganya maskini wa watu wangu haki zao

Misemo hii miwili ina maana moja. "hazina haki kwa maskini na wahitaji miongoni mwa watu wangu"

wahitaji

"watu maskini"

kupora wajane

"chukua kila kitu kutoka kwa wanawake ambao waume zao wameshakufa"

na kufanya wasio na baba mawindo yao

Isaya inalinganisha yatima kwa wanyama ambao wanyama wengine huwinda na kula. Hii inasisitiza ya kwamba yatima hawana uwezo na waamuzi wanaweza kuwadhuru kiurahisi. "na kuwadhuru watoto ambao hawana wazazi kama mnyama anayemfuata windo lake"

mawindo

wanyama ambao wanyama wengine hutaka kuwshika na kuwala