sw_tn/isa/09/16.md

919 B

Wale ambao wanaongoza watu hawa wanawapotosha

Viongozii kusababisha watu kutotii inazungumziwa kana kwamba viongozi waliwaongoza katika njia isiyo sahihi. "Viongozi wa Israeli wamesababisha watu kutomtii Mungu"

na wale ambao wanaongozwa wanamezwa

Hii ni sitiari ambayo inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. Maana zaweza kuwa 1) "na wale ambao wanaongozwa wanachanganyikiwa" au 2) "na Yahwe huangamiza wale ambao wanaongoza"

kila kinywa kinazungumza vitu vya kipumbavu

Neno "kinywa" lina maana ya mtu. "kila mtu huzungumza vitu vya kipumbavu"

Katika vitu hivi vyote, hasira yake haipungui; badala yake, mkono wake

"Ingawa vitu hivi vyote vimetokea, bado ana hasira, na mkono wake"

mkono wake bado unanyoshwa nje

Isaya anazungumza kana kwamba Yahwe alikuwa mtu ambaye anataka kumpiga mtu mwingine kwa ngumi yake. Hii ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuwaadhibu Israeli. "bado atakuwa tayari kuwaadhibu"