sw_tn/isa/09/01.md

1.6 KiB

Huzuni itaondolewa kutoka kwake ambaye alikuwa katika maumivu makali

Isaya anazungumzia watu ambao wamepotea kiroho kana kwamba walikuwa wakitembea katika giza tupu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataondoa giza kutoka kwake aliyekuwa katika maumivu makali"

Huzuni

Neno hili lina maana ya "giza kidogo au giza tupu".

kwake ambaye alikuwa katika maumivu makali

"yeye ambaye alikuwa akiteseka maumivu makali na huzuni". Huenda hii ni sitiari kwa ajili ya watu wa Yuda

Katika kipindi cha awali aliabisha nchi ya Zabulonii na nchi ya Naftali

"Nchi" ina maana ya watu ambao wanaishi katika eneo. "Kipindi cha nyuma, Bwana aliwashusha waleabuloni na Naftali"

lakini katika kipindi cha baadaye ataifanya iwe tukufu, njia ya baharini, mbele ya Yordani, Galilaya ya mataifa

Hapa "ataifanya" ina maana ya Galilaya ambayo inawakilisha watu wanaoishi kule. "lakini katika siku za usoni, Bwana ataheshimu watu wa Galilaya wa mataifa, ambayo ipo katika barabara kati ya Bahari ya Mediteranea na Mto Yordani"

Galilaya ya mataifa

Hapa "mataifa" yanawakilisha watu kutoka mataifa mengine ambao wanaishi Galilaya. "Galilaya, ambapo wageni wengi huishi"

waliotembea gizani ... walioishi katiika nchi ya kivuli cha kifo

isaya anazungumzia watu kuishi maisha ya dhambi na mateso kwa sababu yake kana kwamba walikuwa wakitembea katika nchi ya giza na yenye kivuli cha kifo.

mwanga mkubwa ... mwanga umewaka

Hapa "mwanga" unawakilisha matumaini na ukombozi.

nchi ya kivuli cha kifo

Msemo "kivuli cha kifo" ni lahaja ambayo ina maana ya giza nene. "nchi yenye giza zito"