sw_tn/isa/07/03.md

1.5 KiB

Maelezo ya Jumla

Isaya anaandika juu ya kile kilichotokea kwake kana kwamba kilitokea kwa mtu mwingine.

Shear-yashubu

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi kwa chini ambayo yanasema, "Jina la Shear-yashubu ina maana ya 'waliobakia watarudi'". Maana inaweza kuwa imempatia matumaini Ahazi.

katika mwisho wa mfereji wa dimbwi la juu

"ambapo maji huingia katika dimbwi la juu"

mfereji

mtaro wa kutengenezwa na mtu au chini mwa chini mwa mlima ambmo maji hutiririka

barabara

barabara laini kama la lami.

shamba la dobi

Maana zaweza kuwa 1) hii ni jina la kufaa ambalo watu waliita shamba au 2) hii ni nomino ya kawaida ambayo watu walitumia kuongea juu y shamba, "shamba la dobi" au "shamba ambapo watu huosha sufu"

shamba la dobi

Dobi huwa ni 1) mwanamume ambaye hufua sufu ambayo mtu kanyoa katika kondoo, "Shamba la Mfuaji wa Sufu" au 2) mwanamke ambaye hufua nguo chafu, "Shamba la Mfuaji wa Nguo"

Mwambie

"Mwambie Ahazi"

usiogope au kutishwa kwa mikia ya moto miwili ya kichiniichini, kwa hasira kali ya Resini na Aram, na ya Peka mwana wa Remalia

Mungu analinganisha Resini na Peka kwa njiti zinazowaka ambao moto wake umezimika na kufanya moshi. Mungu anasisitiza ya kwamba sio vitisho vya kweli. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "usimruhusu Resini na Peka kukutisha; hasira yao katili ni kama kijiti kiwakacho ambacho moto wake umezimika na kuna moshi pekee"

usiogope au kutishwa

Maneno "ogopa" na "tishwa" yana moja na yanaweza kutafsiriwa kama neno moja.