sw_tn/isa/06/13.md

656 B

itaangamizwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "majeshi yataangamiza nchi ya Israeli tena"

kama mvinje na mwaloni inapokatwa na mashina kubaki, mbegu takatifu ipo katika kisiki chake

Tashbihi hii ina maana ya kwamba hata baada ya Yahwe kuangamiza Israeli, atawatenga kando watu kutoka miongoni mwa Waisraeli kumtumikia.

mvinye

aina ya mti wa mwaloni

shina ... kisiki

Shina ni shina nene la mti. Kisiki ni sehemu ya mti ambayo inasalia kwenye ardhi baada ya mti kukatwa chini.

mbegu takatifu

Watu ambao watamtumikia Yahwe baada ya majeshi kuangamiza Israeli inazungumziwa kana kwamba walitengwa kando kama mbegu takatifu.