sw_tn/isa/05/13.md

1.1 KiB

Taarifa ya Jumla

Mistari hii inasema kile kitakachotokea kwa watu kwa sababu hawajamtii Mungu.

watu wangu wamekwenda katika kifungo

Katika unabii vitu ambavyo vitatokea katika siku za usoni mara kwa mara vilimaanisha kana kwamba vilikwisha tendeka. Hii inasisitiza ya kwamba unabii utakuja kuwa kweli hakika. "maadui kutoka nchi zingine zitachukua watu wangu, Israeli, kama watumwa"

kwa ukosefu wa ufahamu

Kile ambacho hawaelewi inaweza kuwekwa wazi. "kwa sababu hawamuelewi Yahwe au sheria yake"

Kuzimu imefanya hamu yake kubwa zaidi na imefungua kinywa chake wazi sana

Msemo huu unazungumzia kuzimu, ambayo hapa ina maana ya kaburi, kwa mnyama ambaye yupo tayari kula wanyama wengine. Inasemekana ya kwamba watu wengi, wengi watakufa. "kifo ni kama mnyama mwenye njaa ambaye amefungua kinywa chake wazi kumeza watu wengi"

watu wao wenye uwezo, viongozi wao, na wale ambao wana furaha miongoni mwao, wanashuka kuzimu

Nabii anazungumzia kuhusu siku za usoni kana kwamba kinatokea sasa. "Watu wengi wa Israeli, watu wake muhimu na watu wa kawaida, viongozi wao na wale wanaofurahia sherehe, wataingia kuzimu"