sw_tn/isa/03/13.md

1.7 KiB

Yahwe husimama kwa ajili ya mashtaka; anasimama kuwashtaki watu

Isaya anazungumzia uamuzi wa Yahwe kudhuru watu kana kwamba Yahwe alikuwa akileta mashtaka halali katika mahakama dhidi ya watu wa Israeli. Sehemu ya pili ya mstari huu una maana hiyo hiyo na sehemu ya kwanza, lakini inasema kikamilifu zaidi. "ni kana kwamba Yahwe amechukua nafasi yake katika mahakama na alikuwa tayari kushtaki watu"

atakuja na hukumu

Hukumu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni kitu ambacho mtu anawez kuleta kwa mtu mwingine. "atatangaza hukumu yake" au "atatamka hukumu yake"

Umeharibu shamba la mizabibu

Hapa "umeharibu" ina maana ya wazee na watawala. Yahwe anazungumzia juu ya watu wake kana kwamba walikuwa shamba la mizabibu. Kama mtu anayeshindwa kutunza shamba la mizabibu ili kwamba mizabibu zishindwe kuzaa matunda, wazee na viongozi wanakatisha tamaa Waisraeli kutomtumikia Mungu. "Watu wangu ni kama shamba la mizabibu, na umeliharibu"

Uporaji kutoka kwa maskini upo katika nyumba zenu

"vitu ulivyochukua kutoka kwa maskini zipo ndani ya nyumba zenu"

maskini

Kivumishi kidogo hiki kinaweza kuwekwa kama kivumishi. "wale ambao ni maskini"

Kwa nini unaponda watu wangu na kusaga nyuso za maskini?

Yahwe anauliza swali hili ili kwamba awashataki viongozi wa watu. Mashtaka haya yanaweza kuelezwa kama kauli. "Nina hasira na nyie watu waovu kwa sababu mnaponda watu wangu na kusaga nyuso za maskini"

unaponda watu wangu

Kufanya watu wangu kuteseka inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kuwaponda na uzito mkubwa sana. "kuwaumiza watu wangu kwa ukatili"

kusaga nyuso za maskini

Kuwafanya watu kuteseka inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kufuta nyuso zao katika ardhi. "kudhuru maskini na kuwafanya wateseke"