sw_tn/isa/01/24.md

1.5 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anaanza kuzungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Kwa hiyo

"Kwa sababu hiyo"

Hili ni tamko la Mungu

Nomino dhahania "tamko" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "hivi ndivyo ambavyo Mungu anatamka"

Nitafanya kisasi dhidi ya washindani wangu, na kujilipiza kisasi dhidi ya adui zangu

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. Maneno "chukua kisasi dhidi ya maadui wangu" huzungumza zaidi juu ya Yahwe kufanya chochote anachohitaji kufanya kwa wale wanaofanya kazi dhidi yake ili aweze kuwa na furaha. Maneno "kujilipiza kisasi dhidi ya adui zangu" yanazungumza zaidi juu ya Yahwe kuadhibu kwa haki adui zake. "Nitaadhibu wale ambao wananipinga" au "Nitafanya kile kinachonipendeza kwa wale wanaofanya kazi dhidi yangu, na nitaadhibu kwa haki adui zangu"

Nitageuza mkono wangu dhidi yako

Hapa "mkono" ina maana ya nguvu ya Mungu ambayo angetumia kuadhibu watu wake. "Nitaanza kutumia nguvu yangu yote dhidi yako"

safisha takataka zako kwa maji magadi

Hapa hatua ambayo Mungu hutoa dhambi za watu wake inazungumziwa kana kwamba anatenganisha chuma kutoka kwa vitu vibaya vilivyochanganywa navyo. Maneno "kwa maji magadi" yanaongeza sitiari nyingine, kwa sababu maji magadi hutumika ndani ya sabuni, sio kusafisha chuma. "na kama vile moto unavyotoa uchafu kutoka kwa fedha, nitatoa uovu wote kutoka miongoni mwao"

takataka

Huu ni uchafu na mambo mengine ambayo watu hutoa kutoka kwenye vyuma ili chuma kiwe safi.