sw_tn/isa/01/23.md

998 B

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shair.

Wakubwa wenu ni waasi

"Viongozi wao wanaasi dhidi ya Mungu"

wenzi wa wezi

"wao ni marafiki wa watu ambao huiba kutoka kwa wengine"

rushwa ... malipo

Watu hutoa "rushwa" kama zawadi kwa watawala wasio waaminifu kwa hiyo watawala hapohapo watatenda kinyume na haki. Watawala hupokea "malipo" kama zawadi kutoka kwa wale hutengeneza faida kutoka kwa sheria zisizo haki ambazo mtawala amezipitisha.

hukimbilia malipo

Mtu anapokuwa na shauku sana mtu ampatie rushwa inazungumzwa kana kwamba malipo yanakimbia na mtu anayafukuza. "kila mtu hutamaniu mtu kumlipa pesa kufanya maamuzi yasiyo ya kweli"

Hawawalindi yatima

"hawawalindi wale ambao hawana baba"

wala maombi ya haki ya mjane hajaji mbele zao

"wala hawasikii pale ambapo wajane huenda kwao kupata msaada dhidi ya wale wanaovunja sheria" au "na hawasaidii wajane wanaokwenda kwao kupata msaada dhidi ya wale wanaovunja sheria"