sw_tn/hos/11/05.md

749 B

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza juu ya Israeli.

Je, hawatarudi nchi ya Misri?

Swali hili linamaanisha kuwa taifa la Israeli watakuwa watumwa tena kama walivyokuwa Misri.

Je, Ashuru haitatawala juu yao kwa sababu wanakataa kurudi kwangu?

Taifa la Israeli litachukuliwa mateka na Ashuru kama matokeo ya kutokuwa waaminifu kwa Bwana.

Upanga utaanguka juu ya miji yao

Hapa "upanga" inawakilisha maadui wa Israeli watakao haribu miji ya Israeli.

kuharibu makomeo ya milango yao

Kuharibu makomeo inamaana ya kuondoa ulinzi wa watu.

ngawa wanaita kwa Aliye Juu

Hapa Mungu anajizungumzia mwenyewe. "Ingawa wataniita mimi, niliye juu"

hakuna mtu atawasaidia

Bwana hataruhusu mtu yeyote awasaidie Israeli kwa sababu wamemuacha.