sw_tn/hos/09/08.md

760 B

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

Nabii ndiye mlinzi wa Mungu wangu juu ya Efraimu

"Mlinzi" hulinda nje ya mji wake kuangalia kama kuna hatari inakuja.

Nabii ndiye mlinzi wa Mungu wangu juu ya Efraimu

Nakala nyingine zimetafsiri sentensi hii kama "Nabii wa Mungu wangu ni mlinzi juu ya Efraimu.

Nabii ni

Hii inamaanisha manabii kwa ujumla ambao Mungu aliwachagua.

Efraimu

"Efraimu" inawakilisha watu wote wa Israeli.

mtego wa ndege ni juu ya njia zake zote

"mtego wa ndege" ni mtego unaotumika kukamata ndege. Hii inamaanisha kuwa watu wa Israeli walifanya kila wanaloliweza kumzuia nabii wa Mungu.

Wamejiharibu wenyewe kama siku za Gibea

"Wana wa Israeli wametenda dhambi na kujiharibu kama walivyofanya huko Gibea zamani"