sw_tn/hos/04/17.md

582 B

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza juu ya Israeli.

Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake

Efraimu ni watu wa kaskazini mwa ufalme wa Israeli. Walichagua kuabudu miungu badala ya Bwana. Bwana anamuamuru Hosea asijaribu kuwarekebisha maana hawatasikia.

watawala wake hupenda sana aibu yao

Viongozi hawaoni aibu ya kile walichokifanya wanapoabudu miungu na kugeuka dhidi ya Bwana.

Upepo utamfunga kwa mabawa yake

Hapa "upepo" unawakilisha hukumu ya Mungu na hasira juu ya taifa la Israeli. Bwana ataruhusu maadui wawashinde watu wa Israeli na kuwachukua mateka.