sw_tn/gen/47/18.md

889 B

wakaja kwake

"watu wakaja kwa Yusufu"

Hatutaficha kwa bwana wangu

Watu wanamtambua Yusufu kama "bwana wangu". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "Hatutajificha kwako, bwana wetu" au "Hatutajificka kutoka kwako"

Hakuna kilichobaki machoni pa bwana wangu

Hapa "machoni" ina maana ya Yusufu mwenyewe. "Hatuna kitu kilichobaki kukupa, bwana wetu"

Kwa nini tufe mbele za macho yake, sisi na nchi yetu?

Neno la "macho" lina maana ya macho ya Yusufu. Watu hutumia swali kuweka msisitizo jinsi walivyo na hamu ya kununua chakula. swali hili linaweza kutasfiriwa kama kauli. "Tafadhali usitazame tu tunavyokufa na nchi yetu inaharibika!"

Kwa nini tufe ... wote sisi na nchi yetu?

Nchi inakuwa haina faida na inaharibika kwa sababu hakuna mbegu ya kupanda; kwa hiyo inazungumziwa kana kwamba nchi itakufa.