sw_tn/gen/45/14.md

571 B

Akaikumbatia shingo ya Benjamini ndugu yake na kulia, na Benjamini akalia shingoni mwake

"Yusufu alimkumbatia ndugu yake Benyamini, na wote wakalia"

Akawabusu ndugu zake wote

Katika kipindi cha zamani cha Mashariki ya Karibu, ilikuwa kawaida kumsalimia jamaa kwa busu.

kulia kwa ajili yao

Hii ina maana ya Yusufu alilia alipowabusu.

Baada ya hayo ndugu zake wakaongea naye

Awali walikuwa na hofu juu yake. Sasa walijisikia wanaweza kuongea naye kwa uhuru. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Baada ya hapo ndugu zake waliongea naye kwa uhuru"