sw_tn/gen/41/44.md

1.1 KiB

Mimi ni Farao, mbali na wewe

Farao anasisitiza mamlaka yake. "Kama Farao, ninaamuru hivi mbali na wewe"

mbali na wewe, hakuna mtu atakayeinua mkono wake au mguu wake katika nchi ya Misri

Hapa "nchi" na "mguu" zina maana ya matendo ya mtu. "hakuna mtu ndani ya Misri ataweza kufanya kitu chochote bila ruhusa yako" au "kila mtu ndani ya Misri lazima akuombe ruhusa kabla hajafanya jambo lolote"

hakuna mtu

Hapa "mtu" ina maana ya binadamu kwa ujumla, iwe wa kiume au wakike.

Zafenathi Panea

Jina la Zafenathi Panea kina maana ya "mfunuaji wa siri"

Akampa Asenathi, binti wa Potifera kuhani wa On, kuwa mke wake

Makuhani wa Misri walikuwa tabaka la juu kabisa na upendeleo. Ndoa hii inaashiria nafasi ya Yusufu ya heshima na upendeleo.

Akampa Asenathi

"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Farao alimpatia Yusufu kuwa mke wake.

binti wa Potifera

"Potifera" ni baba wa Asenathi.

kuhani wa Oni

Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.

Yusufu akaenda juu ya nchi yote ya Misri

Yusufu alisafiri katika nchi kusimamia maandalizi ya ujio wa ukame.