sw_tn/gen/29/15.md

679 B

Je unitumikie bure ... ndugu yangu?

Labani anatumia swali kusisitiza ya kwamba anatakiwa kumlipa Yakobo kwa kumtumika. Swali linawezakutafsiriwa kama kauli. Pia linaweza kuwekwa katika njia ya chanya. "Hakika ni sahihi ya kwamba nikulipe kwa kunitumikia ingawa wewe ni ndugu yangu."

Basi Labani alikuwa

Neno "basi" linatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Labani na binti zake"

Macho ya Lea yalikuwa dhaifu

Maana zaweza kuwa 1) "Macho ya Lea yalikuwa mazuri" au 2) "Macho ya Lea yalikuwa ya kawaida"

Yakobo alimpenda Raheli

Hapa neno "alimpenda" lina maana ya mvuto wa kimahaba kati ya mwanamume na mwanamke.