sw_tn/gen/27/39.md

923 B

kumwambia

"akasema kwa Esau"

Tazama

Hii inaongeza msisitizo kwa kile Isaka anachosema baadae. "Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachokwenda kukuambia"

mbali na utajiri wa nchi

Huu ni msemo unaomaanisha nchi yenye rutuba. "mbali na udongo wenye rutuba"

yako ... nawe

Katika 27:39-40 hivi viwakilishi vipo katika umoja na vina maana ya Esau, lakini kile Isaka anachosema pia kinaashiria kwa vizazi vya Esau.

umande juu angani

"umande" ni matone ya maji yanayounda juu ya mimea wakati wa usiku. Hii inaweza kuwekwa wazi. "umande wa usiku kutoka mbinguni kumwagilia mimea yako"

Kwa upanga wako utaishi

Hapa "upanga" ina maana ya vurugu. "Utaiba na kuua watu ili kupata kile unachohitaji kuishi"

utaiondoa nira yake shingoni mwako

Hii inazungumzia juu ya mtu kuwa na bwana kana kwamba utawala wa bwana juu ya mtu ulikuwa ni nira ambayo mtu anaweza kubeba. "utajifanya huru kutoka kwa utawala wake"