sw_tn/gen/27/36.md

1.1 KiB

Je hakuitwa Yakobo kwa haki?

Esau anatumia swali kuweka msisitizo juu ya hasira yake kwa Yakobo. "Yakobo ni jina sahihi kwa kaka yangu!"

Yakobo

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema: "Jina la Yakobo lina maana ya "yeye akamataye kisigino". Katika lugha ya asili jina la "Yakobo" linatamkika kama neno la "mdanganyifu"

Alichukua ... baraka

Hii inazungumzia kuhusu haki ya mzaliwa wa kwanza kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kukichukua. "Alinidanganya kumpatia mara mbili ya urithia ambayo ningepaswa kupokea kama mzawa wa kwanza!"

sasa amechukua baraka yangu

Hii inazungumzia juu ya baraka kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kuchua. "na sasa amekudanganya kumbariki yeye badala yake"

Je haukuniachia baraka

Esau anajua ya kwamba baba hawezi kumbariki na vitu vile vile alivyombariki Yakobo. Esau anauliza kama kuna kitu kinachosalia kusemwa kwake ambacho Isaka hakusema alipokuwa akimbariki Yakobo.

Je nikufanyie nini mwanangu?

Isaka anatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba hakuna kilichobaki atakachofanya. "Hakuna kitu kingine nachoweza kufanya kwako!"