sw_tn/gen/27/29.md

920 B

wakutumikie ... zako

Hapa hivi viwakilishi vipo katika umoja na vina maana ya Yakobo. Lakini baraka pia inalenga vizazi vya Yakobo.

mataifa yainame

Hapa "mataifa" ina maana ya watu. "watu kutoka mataifa yote yainame"

yainame

Hii ina maana ya kuinama na kutoa heshima na taadhima ya unyenyekevu kwa mtu.

Uwe bwana juu ya ndugu zako

"Kuwa bwana juu ya ndugu zako"

ndugu zako ... wana wa mama yako

Isaka anazungumzia baraka hii moja kwa moja kwa Yakobo. Lakini, inahusika kwa vizazvi vya Yakobo ambao watatawala vizazi vya Esau na vizazi vya ndugu yeyote wa Yakobo ambaye anaweza kuwa naye.

na wana wa mama yako wainame chini yako

"na wana wa mama yako watakusujudu"

Kila anayekulaani na alaaniwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Mungu alaani kila mtu anayekulaani"

kila anayekubariki abarikiwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Mungu abariki kila mtu anayekubariki"