sw_tn/gen/27/05.md

1.3 KiB

Basi

Neno "basi" linaonyesha badiliko la msisitizo kwa Rebeka na Yakobo.

Rebeka akasikia Isaka alipoongea na Esau mwanawe

"Rebeka alimsikia Isaka akizungumza na mwanawe Esau"

Esau akaenda ... kuja nayo

Neno "kwa hiyo" inaweza kuongezwa kuonyesha ya kwamba Rebeka anazungumza na Yakobo kwa sababu ya kile alichosikia, na anaongea naye wakati Esau ameondoka. "Kwa hiyo Esau alipokuwa ameondoka ...kuja nayo"

na Esau mwanawe ... na Yakobo mwanawe

Esau na Yakobo walikuwa wote wawili watoto wa Isaka na Rebeka. Wanaitwa "mtoto wake" na "mwanawe" kusisitiza ya kwamba mzazi mmoja alimpendelea mtoto mmoja juu ya mtoto mwingine.

Tazama

Msemo "tazama hapa" unaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata. "Sikiliza kwa makini"

Akasema, 'Niletee mnyama na unitengenezee chakula kitamu, ili nikile na kukubariki mbele za Yahwe kabla ya kufa kwangu

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika hali isiyo moja kwa moja. Alimwambia Esau "kuwinda mnyama pori, na kumtengenezea nyama tamu anayoipenda". Kisha kabla hajafa, Isaka atambariki Esau mbele ya Yahwe.

'Niletee mnyama

"Niletee mnyama pori utakayemwinda na kumuua"

unitengenezee chakula kitamu

"nipikie nyama tamu ninayoipenda"

kukubariki mbele za Yahwe

"kukubariki mbele ya Yahwe"

kabla ya kufa kwangu

"kabla sijafa"