sw_tn/gen/03/14.md

1.5 KiB

umelaaniwa wewe mwenyewe

"wewe peke yako umelaaniwa." Neno "laana" lipo kwanza kwa Kiebrania ili kuweka msisitizo ya tofauti kati ya baraka ya Mungu kwa wanyama na laana juu ya nyoka. Hii ni laana, au namna ambavyo laana zilitamkwa. Kwa kutamka laana hii, Mungu alifanya itokee.

wanyama wote wa kufugwa na wanyama wote wa mwituni

"wanyama wote wa kufugwa na wanyama wote wa mwitu"

Itakuwa kwa tumbo lako utakwenda

"Utasogea kwenye ardhi kwa kutumiatumbo lako". Maneno "itakuwa kwa tumbo lako" huja kwanza kuweka msisitizo ya tofauti kati ya njia ya wanyama wengine wanavyosogea kwa kutumia miguu yao na njia ya nyoka atakavyotelezateleza kwa tumbo lake. Hii pia ni sehemu ya laana.

mavumbi utakula

"utakula mavumbi". Maneno "ni mavumbi" huja kwanza kuweka msisitizo ya tofauti kati ya mimea juu ya ardhi ambayo wanyama wengine hula na chakula kichafu cha ardhi ambacho nyoka angekula. Hii ni sehemu ya laana.

uadui kati yako na mwanamke

Hii inamaana ya kwamba nyoka na mwanamke wangekuja kuwa maadui.

uzao

"mtoto" au "kizazi". Neno "uzao" linamaanisha nini mwanamume huweka ndani ya nwanamke kusababisha mtoto kukua ndani ya mwanamke. Kama neno la "mtoto" linaweza kumaanisha zaidi ya mtu mmoja, kama neno "vizazi".

Atakujeruhi ... kisigino chake

Maneno "wako" na "wake" yanamaanisha uzao wa mwanamke. Iwapo "uzao" ulitafsiriwa kwa wingi, hii yaweza tafsiriwa kama "watajeruhi .. visigino vyao"; kwa hali hii, "wao" na "yao" hutumika kutafsiri kiwakilishi kimoja.

Atakujeruhi

"ponda" au "kujeruhi" au "shambulia"