sw_tn/gen/01/11.md

1.3 KiB

Na nchi ichipushe mimea

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba mimea ichipuke juu ya ardhi, Mungu alifanya ichipuke. "Mimea na ichipuke juu ya ardhi" au "Mimea na iote juu ya ardhi"

mimea: miche inayotoa mbegu na miti ya matunda izaayo matunda

"mimea, kila mche unaozaa mbegu na kila mti unaozaa matunda" au "mmea. Kuwe na mimea itoayo mbegu na matunda ya miti yazaayo matunda". Mimea hutumika hapa kama msemo wa jumla inaojumlsiha mimea na miti yote.

miche

Hii ni aina ya mimea ambayo ina mashina laini, na sio kama ya mbao

miti ya matunda izaayo matunda ambayo mbegu yake imo ndani yake

miti izaayo matunda yenye mbegu ndani yake

kila kitu kwa namna yake

Mbegu zingezaa mimea na miti ambayo ingekuwa kama zile zilipotokea. Kwa namna hii, mimea na miti zingejizalisha zenyewe.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

Mungu akaona kuwa ni vyema

Hapa "ni" inamaanisha mimea, mazao na miti.

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

siku ya tatu

Hii inamaanisha siku ya tatu ambapo ulimwengu ulianza kuwepo.