sw_tn/dan/11/15.md

1.3 KiB

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli.

Mfalme wa Kaskazini atakuja

Hapa "mfalme wa Kaskazini" anajumuisha na jeshi lake pia. "Jeshi la mfalmw wa Kaskazini litakuja"

kuizingira nchi kwa kuweka vilima

Hii inarejelea kitendo cha kurundika udongo ili wanajeshi waweza kuufikia urefu wa ukuta wa mji iili kuwashambulia. Wanajeshi na watumwa wataweka udongo kwenye vikapu na kuvibeba hadi mahali sahihi, na kuumwaga ili kuinua kilima cha udongo.

Mfalme wa Kaskazini atakuja, kuizingira nchi kwa kuweka vilima

"Mfalme wa Kaskazini" hapa inamaanisha wanajeshi katika jeshi la mfalme, ambao wangefanya kazi halisi ya kutengeneza vilima vya udongo.

ngome

Kuta na vitu vingine vilivyojengwa ili kulinda mji

Hawatakuwa na nguvu za kusimama

Mahali hapa kitendo cha kusimama kinawakilisha uwezo wa kupigana.

yeye ajaye ataenenda kwa kufuata tamaa zake kinyume chake

"Mfalme atakayevamia atafanya kili kitu anachokitaka kinyume na mfalme mwingine."

Atasimama

Mahali hapa kusimama kuna maana ya kutawala

nchi ya uzuri

Hii inarejelea nchi ya Israeli . angalia ulivyotafsiri katika 8:9

uharibifu utakuwa mkononi wake

Mahali hapa "uharibifu" unawakilisha nguvu ya kuharibu. Pia, nguvu ya kuharibu inasemwa kana kwamba kilikuwa ni kitu ambacho mtu anaweza kukishikilia katika mikono yake.