sw_tn/2sa/07/10.md

1.2 KiB

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kueleza ahadi zake kwa Mfalme Daudi kupitia nabii Nathani.

Nitateua mahali

"Nitachagua sehemu"

nitawapanda pale

Yahwe anawafanya watu waishi katika nchi daima na kwa usalama inazungumzwa kama kama angewapanda katika nchi.

na hawatasumbuliwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji: Yaani: "na hakuna atakayewasumbua tena"

kutoka siku

Hapa "siku" inawakilisha kipindi kirefu.

Niliwaamru waamzi

Baada ya Waisraeli kuingia katika nchi ya Kanaani na kabla ya kuwa na wafalme wa kuwatawala, Mungu aliteua viongozi walioitwa "waamzi" kuwaongoza katika nyakati za shida.

Nami nitakupa pumziko kutoka kwa adui zako wote...anakwambia kwamba atakutengenezea nyumba

Yaweza kufasiriwa: "Nami nitampa pumziko kutoka kwa adui zake wote... anamwambia kwamba atamtengenezea nyumba"

Nikupumzisha kutoka kwa adui zako wote

"Nitakupa usalama kutoka kwa adui zako wote." Hapa "pumziko" ni nomino dhahania. Yaweza kuwa: "Nitawafanya adui zako wote waache kukushambulia"

Nitakutengenezea nyumba

Maana hii hapa ya "nyumba" inarejea kwa wazao wa Daudi kuendelea kumiliki katika Israeli. Katika 7:3 Yahwe alimuuliza Daudi ikiwa angemjengea nyumba. Pale "nyumba" inawakilisha hekalu.