forked from WA-Catalog/sw_ulb
44 lines
2.7 KiB
Plaintext
44 lines
2.7 KiB
Plaintext
\id PHM
|
|
\ide UTF-8
|
|
\h Filemoni
|
|
\toc1 Filemoni
|
|
\toc2 Filemoni
|
|
\toc3 phm
|
|
\mt Filemoni
|
|
\c 1
|
|
\cl Sura 1
|
|
\p
|
|
\v 1 Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
|
|
\v 2 na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
|
|
\v 3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
|
|
\p
|
|
\v 4 Wakati wote namshukuru Mungu wangu, ninakutaja katika maombi yangu,
|
|
\v 5 Kwa sababu nasikia kuhusu imani uliyonayo katika Bwana Yesu na upendo ulio nao kwa watakatifu wote.
|
|
\v 6 Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
|
|
\v 7 Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya watakatifu wote imekuwa ikitulizwa nawe.
|
|
\p
|
|
\v 8 Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
|
|
\v 9 lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
|
|
\v 10 Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
|
|
\v 11 Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anatufaa sote, wewe na mimi.
|
|
\p
|
|
\v 12 Mimi nimemtuma akurudie wewe, aliye moyo wangu hasa.
|
|
\v 13 Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niko kifungoni kwa ajili ya injili.
|
|
\v 14 Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
|
|
\v 15 Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele.
|
|
\v 16 Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa. Yeye ni mpendwa hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
|
|
\p
|
|
\v 17 Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
|
|
\v 18 Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
|
|
\v 19 Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe. Mimi nitakulipa pasipo na kukuambia yakua ninakudai wewe binafsi uhai hasa.
|
|
\p
|
|
\v 20 Naamu ndugu, acha nipate faida kutoka kwako katika Bwana; uiburudishe nafsi wangu katika Kristo.
|
|
\p
|
|
\v 21 Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
|
|
\p
|
|
\v 22 Wakati huo huo, andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitarudishwa kwenu.
|
|
\p
|
|
\v 23 Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
|
|
\v 24 na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
|
|
\v 25 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.
|