\v 13 Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niko kifungoni kwa ajili ya injili.
\v 14 Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
\v 15 Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele.
\v 16 Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa. Yeye ni mpendwa hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
\p
\v 17 Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
\v 18 Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
\v 19 Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe. Mimi nitakulipa pasipo na kukuambia yakua ninakudai wewe binafsi uhai hasa.
\p
\v 20 Naamu ndugu, acha nipate faida kutoka kwako katika Bwana; uiburudishe nafsi wangu katika Kristo.
\p
\v 21 Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
\p
\v 22 Wakati huo huo, andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitarudishwa kwenu.
\p
\v 23 Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
\v 24 na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
\v 25 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.