sw_tn/act/front/intro.md

3.6 KiB

UTANGULIZI WA KITABU CHA MATENDO YA MITUME

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Jumla

Muhtasari wa Kitabo cha Matendo ya Mitume

  1. Mwanzo wa kanisa na huduma yake(1:1-2:2:41)
  2. kanisa la kwanza Yerusalemu (2:42-6:7)
  3. kuongezeka kwa upinzani na mauaji ya kishujaa ya Stefano (6:8-7:60)
  4. Mateso ya Kanisa na utume wa Filipo (8:1-40)
  5. Paulo anakuwa Mtume (9:1-131)
  6. Utume wa Petro na Wakristo wa Kwanza Wayunani (9:32-12:24),
  7. Paulo, mtume wa Wayunani, Sheria ya Wayahudi na baraza la viongozi wa kanisa Yerusalemu.
  8. Ongezeko la kanisa katikati mwa inchi za karibu ya bahari Mediterane na Asia Ndogo (16:6-19:20)
  9. Paulo anasafiri Yerusalemu na kuwa mfungwa Roma (19:21-28:31)

Kitabu cha Matendo Ya Mitume kinazungumzia nini?

Kitabu cha Matendo Ya Mitume kinazungumzia habari ya Kanisa la Mwanzo kadiri ya lilivyoongezeka. Kinaashiria vile nguvu za Roho Mtakatifu zilivyosaidia kanisa la Kwanza. Matendo haya yanaanza pindi Yesu alipopaa mbinguni hadi miaka thelathini kutoka hapo.

Ni Jinsi gani jina la kitabo hiki kinafaa kutafsiriwa?

Watafsiri wanaweza kuchagua jina liliyotumiwa zamani kwa mfano, 'Matendo ya Roho Mtakatifu' Ama watafsiiri wanaweza kuchagua jina la waziwazi, kama 'Matendo ya Roho Mtakatifu kupitia kwa mitume'.

Nani aliandika kitabu cha Matendo ya Mitume?

Kitabu hakijamtaja mwandishi ingawa kinaelekezewa Tiofila, yule ambaye Mwinjili Luka anamzungumzia. Kitabu kinazungumzia "sisi" kuashiria kwamba mwandishi wake alisafiri na Paulo. Wasomi wengi wengi wa Biblia wanaamini kwamba ni Luka aliyekuwa akisafiri na Paulo. Ndio maana watu wengi wanaamini kwamba Luka ndiye mwandishi wa hiki kitabu na cha Injili Ya Luka.

Luka alikuwa daktari wa matibabu. Mfumo wake wa maandishi unamuashiria kama mtu aliyekuwa na masomo ya juu sana. Kuna uwezekano mkubwa hakuwa Myahudi. Aliyashuhudia matukio mengi yaliyotajwa katika kitabu cha Matendo.

SEHEMU YA 2:maswala muhimu ya kidini na kitamaduni

Kanisa ni nini

Kanisa na kundi la watu wanaomwamini kristu. Kanisa linajumlisha Wayahudi na wasiyo wayahudi (Wayunani). Matukio ya kitabu hiki kinaonyesha jinsi Mungu anavyolisaidia Kanisa ni. Aliwapa uwezo waumini kuishi kiadilifu kupitia kwa Roho wake Mtakatifu.

SEHEMU YA 3: Maswala muhimu ya Tafsiri

Ni mambo gani muhimu katika maandiko ya Matendo ya Mitume?

Yafuatayo ndio maswala muhimu katika Matendo ya Mitume:

Mistari ifuatayo inapatkana katika tafsiri za kitambo za Bibilia, lakini haiko katika nyaraka bora za kitambo za Bibilia. Tafsiri zingine za kisasa huweka mistari hii kwa mabano (). tafsiri za ULB na UDB huiweka kwa maelezo ya chini (footnote)

  • Fililpo alisema, "Ukiamini na moyo wako wote, unaweza batizwa." Muethiopia akajibu, "Naamini kwamba Yesu ni mwana wa Mungu" (Matendo 8:37).
  • "Lakini Sila aliona vema kubaki pale."(Matendo 15:34)
  • "Tulitaka kumhukumu kwa mujibu wa sheria.Lakini Lisia jemadari akafika akamwondoa mikononi mwetu kwa nguvu." (Matendo 24:6b-8a).
  • " Alipokwisha kusema hayo, Wayahudi wakaenda zao, wakiulizana mengi wao kwa wao." (Acts 28:29).

Katika maandiko yafuatayo,haijulikani yaliyosema maandiko ya awali, Watafsiri watahitajika kuchagua masomo yepi ya kutafsiri. ULB ina masomo ya kwanza lakini masomo yake ya pili yamewekwa kwenye maelezo ya chini.

  • "wakarejea kutoka Yerusalemu" (Matendo 12:25). Matoleo mengine ya Bibilia husema, "Walirudi Yerusalemu (ama huko)."
  • "Aliwavumilia" (Matendo 13:18). Matoleo mengine husema, "Aliwahudumia".
  • "Haya ndiyo Bwana asema, yeye aliyeyatenda haya mambo yaliyojulikana tangu zamano."(Matendo 15:17-18). Matoleo ya awali yasema, "Bwana asema, kwake ambako matendo yake yanajulikana kwanzia zamani."

(See: rc://*/ta/man/translate/translate-textvariants