sw_tn/psa/058/009.md

1.2 KiB

Kabla masufuria yenu hayajajaza moto wa kuchoma wa miiba ... miiba ya kijana na miiba ya kuchoma pamoja

Waovu wanazungumziwa kana kwamba walikuwa matawi ya miti ya miiba, na hukumu ya haraka ya Mungu juu yao inazungumziwa kana kwamba atawapuliza au kuwafagia haraka. "Mungu atawaangamiza watu waovu haraka zaidi ya kimbunga kinavyoweza kupuliza matawi ya miiba yaliyowekwa chini ya sufuria la kupikia na kuchomwa na moto"

yenu

Daudi anazungumza na watu wa Mungu.

mwiba

"matawi ya miiba"

Mwenye haki atafurahi atakapoona

Msemo "mwenye haki" inamaanisha watu wenye haki kwa ujumla. "Watu wenye haki watafurahi watakapoona"

ataosha miguu yake kwenye damu ya waovu

Kuloanisha miguu ya mtu kwa kutembea kwenye damu inazungumziwa kama kuosha miguu katika damu. "wenye haki wataloanisha miguu yao katika damu ya waovu" au "wenye haki watatembea katika damu ya waovu"

ataosha miguu yake kwenye damu ya waovu

Idadi kubwa ya watu waovu wanaokufa inaelezwa kwa kutumia kukuza kwa neno la watu wenye haki kuosha miguu yao katika damu ya watu waovu. "watu wengi sana waovu watakufa hadi wenye haki watakapotembea kwenye damu yao, itaonekana kana kwamba wanaweza kuosha miguu yao humo"