sw_tn/psa/057/007.md

1.0 KiB

Moyo wangu ni thabiti, Mungu, moyo wangu ni thabiti

Kuwa jasiri inazungumziwa kama moyo wa mtu kuwa imara badala ya kutikiswa au kusogezwa kirahisi. Msemo huu unarudiwa kuonesha kuwa ana imani kamili kwa Mungu na hata badilika. "Nina imani kamili kwako, Mungu"

Nitaimba sifa

"Mimi nitaimba sifa kwako, Mungu"

Amka, moyo wangu ulio heshimiwa

Kuamka inaweza kuwa sitiari ya kuanza au kujiandaa kufanya kitu. Moyo unamwakilisha mwandishi wa zaburi au hisia zake. "Amka, moyo wangu ulio heshimiwa, imba sifa kwa Mungu" au "Nina heshima kuamka na kuimba sifa kwa Mungu"

amka, kinanda na kinubi

Mwandishi anazungumza kana kwamba kinanda na kinubi ni watu wanaoweza kuimba sifa kwa Mungu. "Amka, kinanda na kinubu na imbeni sifa kwa Mungu" au "Nitacheza kinanda na kinubi huku ninaimba sifa kwa Mungu"

Nitauamsha alfajiri

Alfajiri inazungumziwa kana kwamba iko hai, na kuamka kabla ya alfajiri inazungumziwa kama kuuamsha. Lengo la kuamka kabla ya alfajiri ni kumsifu Mungu. "Nitaamka kabla ya alfajiri" au "Nitaamka kabla jua halijachomoza"