sw_tn/psa/055/022.md

1.3 KiB

Weka mizigo yako

Hapa mwandishi anazungumza na watu wanyofu wengine.

Weka mizigo yako kwa Yahwe

Hapa taabu zinazungumziwa kana kwamba ni mizigo ambayo watu wanatakiwa kubeba. Kumtumaini Mungu kutusaidia wakati tuna shida inazungumziwa kama kumwekea mizigo yetu juu yake ili atubebee. "Mpe Yahwe shida zako" au "Mwamini Yahwe kukusaidia na taabu zako zote kama mtu anavyomwamini mtu mwenye nguvu zaidi kubeba mzigo wake"

atakuchukua

Kumtunza mtu au kumsaidia mtu akiwa na shida inazungumziwa kama kumsaidia. "atakutunza" au "atakulinda"

kamwe hataruhusu mtu mwenye haki kupepesuka

Mtu ambaye anataka kudhuriwa vibaya na maafa fulani inazungumziwa kana kwamba anapepesuka au kuyumba na anataka kuanguka. "hatamuacha mtu mwenye haki ayumbe na kuanguka" au "hataacha mtu mwenye haki aangamizwe"

Lakini wewe, Mungu

Mwandishi anazungumza na Yahwe sasa.

shimo la uharibifu

Hii inaweza kumaanisha kaburi au jahannamu.

utawaleta waovu chini kwenye shimo la uharibifu

Hii inawakilisha kuwasababisha watu kufa. "utawasababisha waovu wafe" au "utawasababisha watu waovu kufa na kwenda sehemu ambapo wafu wapo"

wenye kiu ya damu na watu waongo

"watu wanadanganya na wanaotaka kuwaua wengine" au "wauaji waongo"

hata nusu ya urefu wa wengine

hata nusu ya urefu wa uhai wa wengine