sw_tn/psa/055/020.md

1.3 KiB

ameinua mikono yake dhidi ya wale

Kuinua mkono dhidi ya watu inawakilisha kuwashambulia. Hii inaweza kuwa sitiari ya kusema vitu vinavyowaweka watu katika hatari au kuwasababisha kuwa katika shida. "amewashambulia wale" au "amewasiliti wale"

Mdomo wake

"Mdomo" wa mtu unawakilisha anachosema. "Kile ambacho rafiki yangu amesema"

Mdomo wake ulikuwa laini kama siagi

Maneno yanayopendeza au mazuri kusikia yanazungumziwa kana kwamba ni malaini na mepesi kumeza. "Alichosema kinapendeza kama siagi laini" au "Alisema vitu vizuri"

uhasama

"ovyo" au "chuki"

maneno yake

"Maneno" ya mtu yanawakilisha anachosema. "Alichosema"

maneno yake yalikuwa laini kuliko mafuta

Watu huweka mafuta kwenye ngozi zao kuifanya ijisikie vizuri, na huweka kwenye vidonda kuviponya. Maneno yaliyo yenye huruma au yenye msaada yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa laini au ya kumbembeleza. "aliyosema yalikuwa yenye huruma na ya kumbembeleza kama mafuta" au "alisema vitu venye huruma"

yalikuwa panga zilizo chomolewa

Maneno yanayosababisha shida kwa watu yanazungumziwa kana kwamba ni panga zinazoweza kuumiza watu. "kile alichosema kiliwaumiza watu kama panga zilizochomolewa zifanyavyo" au "alichosema kiliwasababishia watu shida"

panga zilizo chomolewa

Neno "chomolewa" hapa linamaanisha kuwa panga zimetolewa kwenye makasha yake tayari kwa kutumiwa.