sw_tn/psa/053/004.md

1.1 KiB

Je wale wanaotenda udhalimu hawana uelewa - wale ... Mungu?

Swali hili linatumika kuonesha mshtuko ambao mwandishi anahisi kwa sababu watu wanatenda dhambi sana. Inaweza kuandikwa kama kauli mbili. "Wale wanaotenda udhalimu kana kwamba hawajui chochote. Wanawameza watu wangu kana kwamba wanakula mikate, na hawamwiti Mungu!

wale wanao wameza watu wangu kana kwamba wanakula mkate

Kuangamiza watu inazungumziwa kama kuwameza. Kufanya kana kwamba walikuwa wakila mikate inaashiria kuwa walifanya kwa urahisi sana bila kuhisi hatia. "wale wanaowaangamiza watu wangu kwa uhuru kana kwamba wanakula mikate"

Mungu ataitawanya mifupa ya yeyote atakayeweka kambi dhidi yako

Kutawanya mifupa ya watu inamaanisha kuwaua na kuruhusu mifupa yao kubaki walipofia na bila kuwazika vizuri. "Mungu atamwangamiza kabisa yeyote atakaye weka kambi dhidi yako, na mifupa yao italala imetawanyika kwenye ardhi"

yeyote atakayeweka kambi dhidi yako

Kuweka kambi dhidi ya watu inamaanisha kuwashambulia. Majeshi ya adui yalikuwa yakisafiri na kuweka kambi na kuishi kwa muda karibu na watu waliotaka kuwavamia. "yeyote atakaye wavamia"