sw_tn/psa/052/001.md

1.5 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Katika zaburi hii anayezungumziwa ni Doegi. Wakati Sauli alipotaka kumuua Daudi, Doegi alimwambia Sauli mahali alipokuwa Daudi ili Sauli ampate.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Doegi ... Mwedomi

Haya ni majina ya wanaume.

Kwa nini unajivunia kufanya fujo, wewe mwanamme shujaa?

Swali hili linaonesha jinsi Daudi alivyokuwa na hasira na yule aliyeleta matatizo. "Hutakiwi kuwa na majivuno sana kwa kutengeneza matatizo, wewe mwanamme shujaa."

wewe mwanamume shujaa

Inawezekana Daudi alikuwa akitumia kejeli alipokuwa anamwita Doegi hivi. "wewe, unadhani una uwezo sana"

Uaminifu wa agano wa Mungu unakuja

Daudi anazungumzia uaminifu wa Mungu wa agano kana kwamba ni kitu kilichoweza kuja. Inawezekana alikuwa akimaanisha ahadi za Mungu kuwalinda watu wake na watu waovu. Hii inaweza kuelezwa wazi. "Mungu ni mwaminifu kutunza ahadi za agano lake" au "Mungu huwalinda kwa uaminifu watu wake kutoka kwa watu waovu kama wewe"

wembe mkali

ubapa mkali

Ulimi wako unapanga maangamizi kama wembe mkali, unafanya udanganyifu

Hapa ulimi unalinganishwa na wembe mkali ambao unauwezo wa kusababisha madhara makubwa. "Ulimi wako unadhuru watu kama wembe mkali ufanyavyo, unapopanga maangamizi na kudanganya wengine"

Ulimi wako

Hapa "ulimi wako" unaashiria mtu ambaye Daudi anazungumza naye. "Wewe"