sw_tn/psa/049/003.md

1.1 KiB

Mdomo wangu utazungumza hekima

Hapa neno "mdomo" inamaanisha mtu anayezungumza. "Nitazungumza maneno ya hekima"

kutafakari kwa moyo wangu kutakuwa kwa uelewa

Hapa neno "moyo" linawakilisha akili na mawazo. "mawazo ambayo ninatafakari yatanielekeza kwenye uelewa"

tega sikio langu

Mwandishi anazungumzia kusikiliza kitu kwa makini kana kwamba ni kuinamisha sikio la mtu kwa mtu anayezungumza. "sikiliza kwa makini"

kwa kinubi

"kama ninavyocheza kinubi"

Kwa nini niogope ... visigino vyangu?

Mwandishi anatumia wali hili kuweka mkazo kwamba hakuna sababu ya kuogopa vitu vibaya vinapotokea. "Sina sababu ya kuogopa ...visigino vyangu."

siku za uovu

"vitu viovu vikitokea." Hapa neno "siku" linamaanisha nyakati kwa ujumla.

udhalimu unaponizunguka katika visigino vyangu

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi anazungumzia hamu za uovu za adui zake kana kwamba ni mnyama anayewinda wanyama wengine aliye tayari kumpita. "wakati udhalimu wa watu wenye dhambi unapokuwa tayari kunishinda" au 2) adui wa mwandishi wanamzunguka wakati wanatenda udhalimu wao. "adui zangu wanaponizunguka"