sw_tn/psa/048/009.md

777 B

katikati ya hekalu lako

"kama tulivyo kwenye hekalu lako"

Kama jina lako lilivyo ... ndivyo ilivyo sifa yako hadi mwisho wa dunia

Hapa neno "jina" linawakilisha tabia ya Mungu na sifa yake. Misemo hii miwili inalinganisha ukuu wa sifa ya Mungu na jinsi watu wanavyomsifu sana. "Jina lako ni kuu sana ... na kwa hiyo watu duniani kote wanakusifu sana" au "Watu duniani kote wamesikia kukuhusu ... kwa hiyo watu duniani kote wanakusifu"

hadi mwisho wa dunia

Huu ni msemo wa nahau unaomaanisha sehemu zote duniani.

mkono wako wa kuume umejaa haki

Mwandishi anazungumzia haki kana kwamba ni kitu ambacho Mungu anaweza kushika mkononi mwake. Hapa neno "mkono" unamaanisha uwezo na mamlaka ya Mungu kutawala. "unatawala kwa haki" au "wewe ni mwenye haki unapotawala"