sw_tn/psa/048/007.md

1.3 KiB

Na upepo wa mashariki unavunja meli za Tarshishi

Maana zinazowezekana ni 1) hii ni sitiari ambayo mwandishi anawaelezea wafalme kuwa na hofu kana kwamba ni meli zinazotikisika kwa sababu Mungu anaziangamiza kwa upepo mkali. "Walitikisika kwa hofu, kama meli za Tarshishi zinavyotikisika unapozivunja na upepo wa mashariki" au 2) hii ni alama ya kifupisho ambayo mwandishi anaelezea nguvu kuu ya Mungu.

upepo wa mashariki

Maana zinazowezekana ni 1) "upepo unaopuliza kutoka mashariki" au 2) "upepo mkali."

meli za Tarshishi

Maana zinazowezekana ni kuwa hii inamaanisha 1) meli zinazosafiri kwenda Tarshishi au zimetengenezwa katika mji wa Tarshishi au 2) meli yoyote kubwa ya kwenda baharini.

Kama tulivyosikia

Inadokezwa kuwa kile walichosikia ni mambo makubwa ambayo Mungu ametenda kipindi cha nyuma. "Kama tulivyosikia kuhusu mambo makubwa ambayo Mungu ametenda"

ndivyo tulivyoona

Hii inamaanisha kuwa wameona kithibitisho kuwa vitu walivyosikia ni vya kweli. "kwa hiyo tumeona Mungu akifanya mambo makuu sasa"

katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu

Misemo hii miwili inamaanisha Yerusalemu. "katika mji wa Mungu wetu, Yahwe wa majeshi"

imarisha

"ifanye kuwa imara." Hapa neno "imarisha" linamaanisha kutunza na kufanya kitu kuwa salama.