sw_tn/rev/13/01.md

771 B

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza mnyama anayetokea katika maono yake. "nikaona" inamaanisha ni Yohana aliyeona.

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka linatambulika pia katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

Yule joka akampa nguvu zake

Joka alimfanya mnyama kuwa na nguvu kama yeye. Ingawa hakupoteza nguvu zake kwa kumpa mnyama nguvu.

nguvu ... kiti chake cha enzi, na mamlaka yenye nguvu sana ya kutawala

Hizi ni njia tatu zakumaanisha mamlaka yake, na pamoja zinasisitiza kuwa mamlaka yake walikuwa makubwa.

kiti chake cha enzi

"kiti cha enzi" hapa inamaanisha mamlaka ya joka kutawala kama mfalme. "mamlaka yake ya kifalme" au "mamlaka yake kutawala kama mfalme"