forked from WA-Catalog/sw_tn
783 B
783 B
Kauli Unganishi:
Malaika wa mwisho wa wale saba anaanza kupuliza tarumbeta yake.
malaika wa saba
Huyu ni malaika wa mwisho kati ya wale saba. "malaika wa mwisho" au "malaika namba saba"
sauti kubwa zilinena mbinguni na kusema
Usemi "sauti kubwa" huwakilisha wananenaji wanaozungumza kwa sauti kubwa. "Wasemaji mbinguni wakanena kwa sauti kubwa na kusema"
Ufalme wa dunia
Hapa inamaanisha mamlaka ya kutawala ulimwengu. "Mamlaka ya kutawala dunia"
dunia
Hii inamaanisha kila mtu duniani. "kila mtu duniani"
ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake
Neno "ufalme" hapa linamaanisha mamlaka ya Bwana wetu na Kristo wake waliyonayo kutawala.
Ufalme wa dunia umeshakuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake
"Bwana wetu na Kristo wake sasa ni watawala wa dunia"