sw_tn/rev/07/15.md

37 lines
1.4 KiB
Markdown

# Kauli Unganishi:
Mzee aendelea kuzungumza na Yohana.
# wako ...yao ... wao
Hizi zote zinamaanizha wale watu waliotoka katika Dhiki Kuu.
# usiku na mchana
Sehemu hizi mbili na siku zinatumika pamoja kumaanisha "wakati wote" au " bila kukoma"
# atasambaza hema yake juu yao
"ataweka hema yake juu yao." Kuwalinda inazungumziwa kama kuwapa hifadhi ya kuishi. "atawahifadhi" au "atawalinda"
# Jua halitawachoma
Joto la jua linalinganishwa na adhabu inayosababisha watu wateseke. "Jua halitawachoma" au "Jua halitawadhoofisha"
# Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi
"Mwanakondoo anayesimama katikati ya eneo ya kiti cha enzi" au "Mwanakondoo aliye katika kiti cha enzi"
# Kwa kuwa Mwanakondoo ... atakuwa mchungaji wao
Wazee wanamzungumzia Mwanakondoo kuwajali watu wake kama mchungaji anavyojali kondoo wake. "Kwa kuwa Mwanakondoo ... atakuwa kama mchungaji kwao" au " Kwa kuwa Mwanakondoo ... atawajali kama mchungaji anavyojali kondoo wake"
# atawaongoza katika chemchemi ya maji ya uzima
Wazee wanakizungumzia kinachowapa uhai kama vile ni chemchemi ya maji safi. "Atawaongoza kama mchungaji awaongozavyo kondoo wake kwenye maji masafi" au "atawaongoza kuelekea maishani kama mchungaji anavyowaongoza kondoo wake kuelekea kwe maji masafi"
# Mungu atafuta kila chozi katika macho yao
Machozi hapa yanawakilisha huzuni. "Mungu atafuta huzuni yao kama vile anafuta machozi yao" au "Mungu atawasababisha wasiwe na huzuni tena"