sw_tn/psa/105/043.md

627 B

Akawaongoza watu wake nje ... wateule wake kwa kelele za ushindi

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kusisitiza ya kwamba watu wa Mungu walikuwa na furaha alipowaongoza kutoka Misri. Watu walikuwa wakipiga kelele kwa furaha. "Aliwaongoza watu wake wateule kwa kelele za furaha na ushindi"

wateule wake

Hapa "wateule" ina maana ya watu wateule wa Yahwe. "watu wake wateule"

ushindi

"sherehe" au "furaha"

kuzishika amri zake na kutii sheria zake

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kwa ajili ya msisitizo. "Kushika" amri zake ina maana ya kuzitii. "kutii sheria zake na maagizo"