1.1 KiB
Wale walio barikiwa na Mungu
"Wale ambao Mungu anawabariki"
watarithi nchi
Umiliki wa nchi unazungumziwa kanakwamba umepokelewa kama urithi. "watapokea nchi kama mali yao" au "wataruhusiwa kuishi kwa usalama katika nchi"
wale waliolaaniwa naye
"wale ambao Yahwe amewalaani"
watakatwa
Uharibifu wa watu waovu unazungumziwa kana kwamba ni tawi la mmea uliokatwa na kutupwa.
Ni kupitia Yahwe hatua za mtu zinaimarishwa ... inpendeza machoni pa Mungu
"Kama mtu anaishi katika njia ya kupendeza machono pa Yahwe, Yahwe ataimarisha njia zake"
Ni kupitia Yahwe hatua za mtu zinaimarishwa
"Yahwe ndiye anayemwezesha mtu kufanikiwa"
mtu ... mtu
Hii haimaanishi mtu bayana, lakini kwa watu kwa ujumla.
hatua za mtu
Hatua zinawakilisha jinsi mtu anavyoishi. "jinsi mtu anavyoishi"
Ingawa anajikwaa, hataanguka
Hapa "kujikwaa" na "kuanguka" inamaanisha jinsi mtu anavyojibu katika vipindi vigumu. "Ingawa ana vipindi vigumu, hatashindwa kabisa"
anamshika kwa mkono wake
Hapa "mkono wake" inamaanisha nguvu ya Yahwe, na "kumshika" inamaanisha kumlinda. "kumlinda na nguvu yake"