sw_tn/psa/025/001.md

1.1 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

nainua maisha yangu

Msemo "nainua maisha yangu" ni sitiari. Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi unajitoa kwa Yahwe, ambayo inamaanisha anamtegemea Yahwe kabisa. "nitajitoa kwako" au 2) aleta maombi na heshima kwa Yahwe. "ninakuabudu na kukuheshimu"

Usiniache niaibike

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Usiwaache adui zangu waniaibishe"

niaibike

"kudhalilika"

wafurahi kwa ushindi juu yangu

Msemo "juu yangu" unadokeza kuwa adui zake wamemshinda na kusima juu kwa ushindi. "wanishinde na kufurahia"

Na mtu yeyote anayekutumaini asiaibike

"Usiwaache wale wanaokutumaini waaibike." Aibu inaweza kuja kwa kushindwa na dui zao. Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "Usiwaache adui wawashinde wale wanaokutumaini"

anayekutumaini

"wanaokuamini"

fanya udanganyifu

"fanya uongo" au "fanya ujanja"

bila sababu

"bila chanzo"