sw_tn/psa/019/004.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla:

Daudi amemaliza tu kusema kuwa uumbaji unaonesha utukufu wa Mungu.

maneno yao ...kusema kwao

Hii namaansiha "maneno" yasiyozungumzwa ya uumbaji yanayoonesha utukufu wa Mungu.

maneno yao huenda

Maneno yanaelezwa kana kwamba ni watu ambao wanatoka na ujumbe. "maneno amabyo uumbaji unazungumza ni kama watu wanaoenda nje"

kusema kwao hadi mwisho wa dunia

"kusema kwao kunaenda hadi mwisho wa dunia"

Ameweka hema kwa ajili ya jua

Hapa mwandishi anazungumzia sehemu ambayo Yahwe aliumba kwa ajili ya jua kana kwamba ni hema. "Aliumba sehemu kwa ajili ya jua"

miongoni mwao

Neno "mwao" inaweza kuwa inamaanisha mbingu.

Jua ni kama bwana arusi anayetoka katika chumba chake

Mwandishi anazungumzia kuchomoza kwa jua kana kwamba ni bwana arusi. "jua ni kama bwana arusi akitembea kwa furaha kwenda kwa bibi arusi wake"

kama mwamme menye nguvu anayefurahi anapokimbia mbio yake

Hii inalinganisha jua na mwanariadha kusisitiza nguvu na mwanga wa jua.

mwanamme mweye nguvu

"mkimbiaji mwenye kasi"

upeo wa macho

mstari ambao ardhi na anga hukutana

hadi mwingine

Hapa "mwingine" inamaanisha upeo wa macho. "hadi kwenye upeo wa macho mwingine"

hakuna kinachotoroka joto lake

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "kila kitu kinahisi joto lake"